Home LOCAL SERIKALI KUSIMAMIA UANDAAJI WA BAJETI UNAOZINGATIA JINSIA

SERIKALI KUSIMAMIA UANDAAJI WA BAJETI UNAOZINGATIA JINSIA


Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu) Bwa. Kaspar Mmuya (katikati) akizungumza wakati wa ufunguzi wa mafunzo ya Uandaaji wa Bajeti zinazozingatia Usawa wa Kijinsia kwa Wakurugenzi na Wakuu wa Vitengo kutoka ofisi hiyo (mwisho) ni Mkurugenzi Msaidizi Idara ya Sera, na Uratibu wa Shughuli za Serikali Bwa. Crispin Musiba na (wa kwanza kulia) ni Mratibu Taifa wa Mradi wa Kutokomeza Ukatili dhidi ya Wanawake na Watoto (MTAKUWWA) Bi.Happiness Mugyabuso yaliyofanyika Aprili 20, 2022 Ukumbi wa Ofisi hiyo Dodoma.

Mwezeshaji kutoka Sekretarieti ya Mpango Kazi wa Taifa wa Kutokomeza Ukatili dhidi ya Wanawake na Watoto (MTAKUWWA) Bwa. Joel Mangi ambaye pia ni Mchumi Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum akiwasilisha taarifa ya Hali ya Utekelezaji wa MTAKUWWA katika mafunzo hayo Aprili 20, 2022 Dodoma.
Mtalaamu wa masuala ya Jinsia, Haki za Binadamu na HUduma za Jamii kutoka Mtandao wa Jinsia Tanzania (TGNP) Bi.Gemma Akilimali akiwasilisha Historia ya Bajeti kwa mtazamo wa Kijinsia katika mafunzo ya Uandaaji wa Bajeti zinazozingatia Usawa wa Kijinsia kwa Wakurugenzi na Wakuu a Vitengo kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge na Uratibu) yaliyofanyika Aprili 20, 2022 Ukumbi wa Ofisi hiyo Dodoma.
Afisa Mradi Mwandamizi kutoka Shirika lisilo la Kiserikali la Women Fund Tanzania-Trust (WFT-T) BI. Neema Msangi akieleza jambo wakati wa mafunzo ya Uandaaji wa Bajeti zinazozingatia Usawa wa Kijinsia yaliyotolewa kwa Wakurugenzi na Wakuu wa Vitengo kutoka (Ofisi ya Waziri Mkuu Sea, Bunge na Uratibu) (kulia) ni Mkurugenzi Msaidizi Idara ya Utawala na Rasilimali Watu Ofisi ya Waziri Mkuu yaliyofanyika Aprili 20, 2022 katika Ukumbi wa Ofisi hiyo Dodoma.
Baadhi ya Washiriki wakifuatilia mafunzo ya Uandaaji wa Bajeti zinazozingatia Usawa wa Kijinsia yaliyotolewa kwa Wakurugenzi na Wakuu wa Vitengo kutoka (Ofisi ya Waziri Mkuu Sea, Bunge na Uratibu) yaliyofanyika Aprili 20, 2022 katika Ukumbi wa Ofisi hiyo Dodoma.

Na: Mwandishi Wetu- Dodoma

Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge na Uratibu Bw. Kaspar Mmuya amesema serikali itaendelea kusimamia uandaaji wa bajeti unaozingatia masuala ya kijinsia kama sehemu ya mapambano dhidi ya vitendo vya ukatili wa kijinsia kuhakikisha vitendo hivyo vinakomeshwa.

Naibu Katibu Mkuu huyo ametoa kauli hiyo Aprili 20, 2022 wakati akifungua mafunzo ya Uandaaji wa Bajeti zinazozingatia Usawa wa Kijinsia ili kuwajengea uwezo  Wakurugenzi na Wakuu wa Vitengo kutoka ofisi hiyo yaliyofanyika Dodoma ambapo alisema elimu hiyo itasaidia watendaji kuzingatia utengwaji wa bajeti zenye mrengo wa kijinsia kama hatua ya mapambano ya ukatili nchini.

Alifafanua kwamba uzingatiaji wa bajeti zinazozogusa jinsia ni muhimu hasa wakati huu ambapo Wizara mbalimbali zinawasilisha bajeti zao katika  vikao vya Bunge linaloendelea upo umuhimu wa kuhusisha masuala ya jinsia hatua itakayosaidia kutatua changamoto zinazojitokeza.

“Tupo kwenye hatua ya kupeleka bajeti zetu bungeni na baadaye kuridhiwa na Bunge lakini kwenye bajeti hizi yawezekana kuna  eneo muhimu sana ambalo limeguswa au limeguswa kwa kiasi kidogo jicho la kuangalia bajeti zetu Je,zinagusa mtazamo wa jinsia? unavyopanga bajeti unaangalia utekelezaji wake utagusa wanawake? utagusa jinsia nidcho kitu cha msingi hivyo tunaamini mafunzo haya yatatujenga vizuri,”Alisema Bwa. Mmuya.

Vile vile albainisha kwamba mafunzo hayo ni muhimu na yamefanyika wakati muafaka kwa watumishi wa ofisi hiyo huku akizipongeza taasisi na mashirika yanayoiunga mkono serikali kusimamia usalama wananchi na kulinda haki za binadamu utakaochochea ustawi wa raia na Taifa kwa ujumla.

Kwa upande wake Mwezeshaji kutoka Sekretarieti ya Mpango  Kazi wa Taifa wa Kutokomeza Ukatili dhidi ya Wanawake na Watoto (MTAKUWWA) Bwa. Joel Mangi ambaye pia ni Mchumi Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum alitaja baadhi ya sababu ambazo zinasababisha kuendelea kwa matukio ya kikatili ndani ya jamii.

“Utafiti unaonyesha chanzo kimojawapo cha ukatili ni umasikini hususani wanawake,ukosefu wa elimu ,mila na desturi kandamizi wanapokuwa hawajitegemei kiuchuni inachochea ukatili ndani ya familia kwahiyo tukaona tuelimishe jamii kuhusu namna ya kujijenge kiuchuni na katika mila na desturi pia tuliwekeza katika elimu kupinga mila kandamizi kwa wanawake na watoto,”alieleza Mwezeshaji huyo.

Aidha Afisa Mradi Mwandamizi kutoka Shirika lisilo la Kiserikali la Women Fund Tanzania-Trust (WFT-T) Bi. Neema Msangi alisema utengwa kwa bajeti inayozingatia jinsia itasaidia fursa ya kutatua changamoto mbalimbali ambazo huwakabili wananwake na watoto ndani ya jamii.

“Tunapozungumzia bajeti yenye mrengo wa jinsia tutaweza kuona picha halisi ya namna gani tusipotazama bajeti zetu kwa kuzingatia jinsia ziatenda kuwapa shida na watoto ndiyo maana sisi kama WFT-T kwetu tuliona ni nafasi kubwa  na tuliona tuna sababu kabisa ya kuungana na nyie,”alifafanua Afisa huyo.

MWISHO

(PICHA ZOTE NA OFISI YA WAZIRI MKUU)

(SERA, BUNGE NA URATIBU)

Previous articleYASEMAVYO MAGAZETI ALHAMISI YA LEO APRIL 21-2022
Next articleRUWASA MKOANI MTWARA YARUDISHA MATUMAINI YA HUDUMA YA MAJI SAFI NA SALAMA KWA WANANCHI WA NEWALA
Hughes Dugilo is a Writer, News Producer, Video-Photographer Journalist, and Video Editor experienced for 20 years now performing in News, Documentary, Advertisements and Television Programs. Aside from all above he own and operate his Blog known as Green Waves Media TZ since 2018.

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here