Home SPORTS YANGA SC YAENDELEZA UBABE WA USHINDI, YAICHAPA KAGERA SUGAR 3-0 KWA MKAPA

YANGA SC YAENDELEZA UBABE WA USHINDI, YAICHAPA KAGERA SUGAR 3-0 KWA MKAPA

Thank you for reading this post, don't forget to subscribe!



Na: Mwandishi wetu, DAR.

KIKOSI cha Yanga leo kimesepa na alama  tatu dhidi ya Kagera Sugar katika mchezo wa Ligi Luu Bara uliochezwa Uwanja wa Mkapa.
Ni mabao matatu ambayo yamefungwa kwa Yanga inayonolewa na Kocha Mkuu, Nasreddine Nabi.
Fiston Mayele ametupia mabao mawili na pasi moja ya bao, amefunga dk 30 na 50 pasi kampa mshikaji wake Said Ntibanzokiza dk ya 64.
Yanga inafikisha pointi 42 ikizidi kujikita nafasi ya kwanza kwa msimu wa 2021/22.