Home LOCAL MHE. MARY MASANJA AWATAKA WANANCHI KUACHA KUMEGA MAENEO YA HIFADHI

MHE. MARY MASANJA AWATAKA WANANCHI KUACHA KUMEGA MAENEO YA HIFADHI

Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Mary Masanja (Mb) amewataka wananchi kuacha kuomba kumegewa maeneo ya Hifadhi ili kuepukana na changamoto ya wanyamapori wakali na waharibifu.

Amesema hayo leo Wilaya ya Bariadi Mkoani Simiyu wakati Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan alipompa nafasi ya kujibu kuhusu changamoto ya wanyama wakali na waharibifu mkoani humo.

Amesema kuwa ili kukabiliana na changamoto hiyo, vikosi kazi vitatumwa katika maeneo yenye changamoto ya wanyama wakali na waharibifu.

Aidha,ameahidi kutekeleza maelekezo ya Rais ya kuhakikisha Wizara inaweka Kambi ya kudumu kwenye maeneo yenye changamoto ya wanyama wakali na waharibifu.

Previous articleWAANDISHI WA HABARI WATAKIWA KUHAMASISHA CHANJO YA IVIKO 19
Next articleWAZIRI KIJAJI: SERIKALI KUIWEZESHA NDC KUONGEZA UZALISHAJI NA USAMBAZAJI WA VIUAUDUDU VYA KUUA MBU
Hughes Dugilo is a Writer, News Producer, Video-Photographer Journalist, and Video Editor experienced for 20 years now performing in News, Documentary, Advertisements and Television Programs. Aside from all above he own and operate his Blog known as Green Waves Media TZ since 2018.

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here