Home SPORTS ZANZIBAR YANG’ARA TAIFA CUP

ZANZIBAR YANG’ARA TAIFA CUP



NA; STELLA KESSY.

ZANZIBAR imefanikiwa kung’ara katika mashindano ya Taifa Cup yaliyomalizika juzi kwenye Uwanja wa Benjamin Mkapa,Dar Es Salaam.

Katika Soka wanaume  Mkoa Mjini Magharibi ambao wamejipatia zawadi ya shilingi milioni tatu,medali ya dhahabu na.kombe, huku nafasi ya pili  ikienda kwa Mara ambao nao wamepata medali ya shabq shilingi milioni mbili na Kombe  na tatu ilemqliziwa na Ruvuma ilipata medali ya shaba, Kombe na shilingi milioni moja.

Kwa upande wa wanawake wa  Arusha wzlitawazwa kuwa malkia wa mashindano hayo waliojipatia zawadibya Kombe,shilingi milioni tatu na medali ya dhahabu, ikifuatiwa na Dar Es Salaam wakikamata nafasi ya pili kwa kupata zawadi ya shilingi milioni mbili,medali ya fedha na Kombe,huku  Mara wakimalizia nafasi ya tatu wakipata medali ya shaba,Kombe na shilingi milioni moja.

Katika Mchezo wa netiboli Mjini Magharibi walitwaa Ubingwa na kupata medali ya dhahabu,Kombe na shilingi milioni tatu  ,huku nafasi ya pili ikienda kwa Dar Es Salaam wakipata shilingi milioni mbili,medali ya fedha na Kombe ,ikimaliziwa na Dodoma nafasi ya tatu na waliojipatia zawadi ya shilingi milioni moja,medali ya shaba na Kombe.

Kwa mchezo wa riadha Kusini Unguja imeibuka na ubingwa ,huku nafasi ya pili ikienda kwa Arusha na ya tatu ikimaliziwa na Kilimanjaro ambao wamepata makombe.

Katika tasnia ya muziki  wa singeli Mjini Magharibi imemaliza, nafasi ya tatu ,huku nafasi ya pili ikienda Dar Es Salaam na bingwa Morogoro,huku  

Bongo flava wa tatu Dar Es  Salaam ,akifuatiwa na Mbeya alichukua nafasi ya pili, na bingwa  ni Pwani.

Mkurugenzi wa Maendeleo ya Michezo Wizara ya Utamaduni ,Sanaa na Michezo Yusuph ,Singo,alisema kuwa wanamshukuru kwa kuanza na kumaliza salama mashindano hayo.

Alisema kuwa mikakati yao ni kuboresha zaidi mashindano hayo kwa kuongeza michezo ya kushindaniwa kwa wakati ujao.

Singo alisema kuwa kupitia mashindano hayo waajivunia kupata matunda yakiwamo na kurejesha michezo ya pamoja kwa kushirikiana kimuungano .

“Tunashukuru tumemaliza ,lakini kulikuwa na changamoto za hapa na pale na tumeweza kuchukua hatua,kwani mwaka ujao tunataka kuboresha zaidi,” alisema Singo.

Alisema kuwa wamefanikiwa kuibua  na kuvumbua vipaji vipya,huku wanaamini vyama na mashirikisho ya michezo waleweza kuona vipaji ambavyo vitaweza kuingizwa kwenye timu za taifa na kuandaliwa kwa mashindano mbalimbali.

Mashindano hayo yalianza Desemba 10 mwaka huu yalifunguliwa na Waziri Utamaduni,Sanaa na Michezo Innocent Bashungwa na  kufungwa na 

Waziri wa Habari ,Vijana ,Utamaduni na Michezo Zanzibar Tabia Maulid Mwita Desemba 16 mwaka huu.

Previous articleWAZIRI WA MAMBO YA NJE BALOZI MULAMULA KUHUDHURIA MKUTANO WA AFRIKA NA UTURUKI INSTANBUL
Next articleKIKOSI CHA YANGA KUIFUATA PRISONS
Hughes Dugilo is a Writer, News Producer, Video-Photographer Journalist, and Video Editor experienced for 20 years now performing in News, Documentary, Advertisements and Television Programs. Aside from all above he own and operate his Blog known as Green Waves Media TZ since 2018.

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here