Home LOCAL WAHENGA AMEISHAURI SERIKALI KUJENGA SHULE ZA AWALI

WAHENGA AMEISHAURI SERIKALI KUJENGA SHULE ZA AWALI



Na: HERI SHAABAN (ILALA )

WAHENGA ALUMINUM  wameishauri Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa  Tanzania kutenga darasa la  shule za madarasa ya awali kwa ajili ya Wanafunzi kuwandalia mazingira bora ya elimu .

Hayo yalisemwa na Mkurugenzi wa Kampuni ya Wahenga Aluminum John Ryoba leo,wakati wa mahafali ya Kituo cha Day Care  CHADASH kilichopo Kinyerezi  Kibaga Wilayani Ilala .

“Nampongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan kuwekeza katika sekta ya elimu na Sera ya Serikali ya elimu bila malipo  kazi nzuri Serikali imefanya ,naishauri Serikali  iwawekee  watoto Msingi imara katika sekta ya elimu kwa kuanzisha shule za awali nchi zima “ alisema Ryoba 

Mkurugenzi wa Wahenga Ryoba alisema watoto wanapoanzia madarasa ya awali inawajengea kujiamini pamoja na maadili mazuri darasani hivyo wazazi wawapeleke watoto madarasa ya awali kabla elimu ya Msingi. 

Ryoba alisema watoto wanapoanzia darasa la awali wanakuwa na msingi imara wa kuwaongoza darasani mpaka chuo kikuu .

Akizungumzia Kituo cha Day Care Chadash Ryoba alisema amewapongeza Kituo  kina mazingira bora amewataka wawekeze katika elimu ya Msingi mpaka chuo kikuu ili watanzania wasome katika chuo hicho na wageni mbalimbali.

Alisema Taifa lolote liweze kusonga mbele   na kuwa na Maendeleo lazima watu wake wasome na kupata elimu bora sio bora elimu amewataka wadau kuwekeza katika elimu

Kwa upande wake Mkurugenzi wa Kituo cha Day Care CHADASH Kokwihukya Kaino  alisema  Chadash Day Care ilianzishwa mwaka 2020 na kusajiliwa na Serikali  kwa sasa ina Wanafunzi 25.

Mkurugenzi wa CHADASH Day Care alielezea changamoto za barabara mpaka kufika eneo hilo shule hiyo ameomba Serikali iwaboreshee miundombinu.

Mwenyekiti wa Serikali za Mtaa Kibaga Hashimu Kulana amewataka Wazazi kuzingatia katika sekta ya elimu kwa kusomesha watoto kuanzia elimu ya Msingi mpaka chuo Kikuu .

Mwenyekiti Hashimu alisema Wazazi wasio na uwezo ofisi yake ya Serikali za Mitaa itagharamia vifaa vya shule kwa Wanafunzi wa Mtaa Kibaga.

Mwisho

Previous articleJOKATE AIPONGEZA PUMA ENERGY TANZANIA KWA KUTOA AJIRA KWA VIJANA WA KITANZANIA
Next articleMASHABIKI WA YANGA SC WAMIMINIKA KUCHANGIA DAMU MOI, WAKUSANYA CHUPA ZAIDI 100
Hughes Dugilo is a Writer, News Producer, Video-Photographer Journalist, and Video Editor experienced for 20 years now performing in News, Documentary, Advertisements and Television Programs. Aside from all above he own and operate his Blog known as Green Waves Media TZ since 2018.

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here