Home SPORTS WAZAZI WILAYA ILALA KUJENGA NYUMBA YA MTUMISHI

WAZAZI WILAYA ILALA KUJENGA NYUMBA YA MTUMISHI

Na: Heri Shaaban.

JUMUIYA ya Wazazi Wilaya imeanza mikakati ya kujenga nyumba ya  Katibu wa Wazazi wa Wilaya Ilala.

Mkakati huo  umenza hivi  karibuni  kufuatia Mtumishi wake kukosa nyumba  kuishi.

Akizungumza katika Bonanza la Wazazi Dar Salam Mwenyekiti  wa Wazazi Wilaya ya Ilala , Mohamed Msophe 

alisema mkakati huo wa kujenga umeanza hivi karibuni kwa kushirikiana  na Wadau wa maendeleo na wenye mapenzi mema na chama.

“Chama ni chetu ,Jumuiya hii ni yetu tunawaomba wadau wa maendeleo ,na wenye mapenzi mema ya chama   eneo letu lipo Buyuni la Jumuiya yetu ya Wazazi ndio tutajenga nyumba ya mtumishi wetu Katibu wa Wilaya taratibu zote zimeanza hivi karibuni tutazindua rasmi  nawaomba tushirikiane kwa pamoja  kusaidia Chama na Jumuiya yetu ” alisema Msophe .

Msophe aliwaomba wadau waliokuwa tayari kuchangia wawasilishe Wilayani ofisi za Jumuiya ya Wazazi watapewa taratibu zote namba ya kulipia akaunti ya Jumuiya ya Wazazi Contro namba.

Akizungumzia Bonanza la Michezo alisema dhumuni lake kuwaita wanachama wote wa Jumuiya ya Wazazi kuwasajili katika utaratibu unaotambulika waweze kuwatambua kwa ajili ya kuunda vikundi kila kata kwa ajili ya kuwainua kiuchumi waweze kupata mikopo ya Serikali wajiwezeshe kiuchumi .

“Siasa na Uchumi kila kata  Jumuiya yetu inatakiwa wabuni miradi ya maendeleo itakayowawezesha jumuiya yetu kusimama imara “ alisema .

Mwenyekiti wa Bonanza Wilaya ya Ilala Shamsudini Hemed alisema Bonanza hilo limeshirikisha michezo yote ya kuvuta  kamba ,magunia ,kukimbiza kuku ,mpira wa miguu Wanawake na Wanaume.

Shamsudini alisema  katika bonanza hilo wametoa zawadi mbalimbali kwa mabingwa ikiwemo ,Mbuzi ,jezi na mipira kwa ajili kwa Washindi.

Mjumbe wa Mkutano Mkuu MNEC Wazazi Taifa Selemani Juma Kimea  alipongeza Jumuiya ya Wazazi Wilaya ya Ilala kwa kubuni jambo kubwa kuweka Jumuiya Pamoja kwa ajili ya kujenga Chama na jumuiya zake

MNEC Selemani Juma Kimea alisema michezo ina jenga Afya udugu na Mshikamano hivyo aliwataka Jumuiya ya Wazazi Wilaya ya Ilala pamoja na Wanachama wake kujenga umoja na mshikamano kwa ajili ya kujenga chama na kukitangaza chama.

Mwisho

Previous articleSERIKALI, UNESCO YAKUTANISHA WADAU KUJADILI MKAKAKATI WA KUTOKOMEZA UKATILI KWENYE VYUMBA VYA HABARI
Next articleTANZANIA, MSUMBIJI NANI MBABE LEO FAINALI COSAFA
Hughes Dugilo is a Writer, News Producer, Video-Photographer Journalist, and Video Editor experienced for 20 years now performing in News, Documentary, Advertisements and Television Programs. Aside from all above he own and operate his Blog known as Green Waves Media TZ since 2018.

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here