Home LOCAL RAIS DK.MWINYI AFUNGUA MASIKITI WA MASJID AL NOOR UNGUJA UKUU KAEPWANI NA...

RAIS DK.MWINYI AFUNGUA MASIKITI WA MASJID AL NOOR UNGUJA UKUU KAEPWANI NA KUJUMUIKA KATIKA IBADA YA SALA YA IJUMAA

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk.Hussein Ali Mwinyi akisalimiana na Viongozi wa Masjid Al-Noor Unguja Ukuu Kaepwani alipowasili katika viwanja vya Msikiti huo kwa ajili ya ufunguzi wake baada ya kukamilika ujenzi wake na kujumuika na Wananchi wa Kijiji hicho katika Ibada ya Sala ya Ijumaa.

  RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Alhaj Dk.Hussein Ali Mwinyi akiondoa pazia kuashiria kuweka Jiwe la Msingi la Ufunguzi wa Masjid Al-Noor Unguja Ukuu Kaepwani Wilaya ya Kati Unguja na (kulia ) Sheikh Feisal Al Kindi na Mkuu wa Mkoa wa Kusini Unguja Mhe Rashid Hadid Rashid, na kujumuika na Wananchi wa Unguja Ukuu katika Ibada ya Sala ya Ijumaa iliofanyika katika msikiti huo leo


RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk.,Hussein Ali Mwinyi akikata utepe kuashiria kuufungua Msikiti wa Masjid Al-Noor Unguja Ukuu Kaepwani Wilaya ya Kati Unguja na (kulia kwa Rais) Msimamizi wa Ujenzi wa Msikiti huo Sheikh Feisal Al-kindi na (kushoto kwa Rais) Mkuu wa Mkoa wa Kusini Unguja Mhe. Rashid Hadid Rashid, hafla ya ufunguzi huo iliyofanyika.


WANANCHI wa Kijiji cha Unguja Ukuu Kaepwani Wilaya ya Kati Unguja wakimsikiliza Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk.Hussein Ali Mwinyi akizungumza na kuwasalimia baada ya kumalizika kwa Ibada ya Sala ya Ijumaa iliyofanyika katika Masjid Al Noor Unguja Ukuu Kaepwani,baada ya kuufungua rasmin msikiti huo
.
 
RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk.Hussein Ali Mwinyi akizungumza na kuwasalimia Wananchi wa Kijiji cha Unguja Ukuu Kaepwani Wilaya ya Kati Mkoa wa Kusini Unguja, baada ya kumalizika kwa Ibada ya Sala ya Ijumaa na hafla ya ufunguzi wa Masikiti wa Masjid Al Noor Unguja Ukuu Kaepwani, baada ya kukamilika kwa ujenzi wake.


RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhaj Dk.Hussein Ali Mwinyi akisalimiana na kuagana na Viongozi wa Dini baada ya kumalizika kwa hafla ya Ufunguzi wa Masjid Al Noor Unguja Ukuu Kaepwani Wilaya ya Kati Unguja na Ibada ya Sala ya Ijumaa iliyofanyika katika Masjid hiyo.


RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Alhja.Dk.Hussein Ali Mwinyi akifurahia jambo wakati akiagana na Viongozi wa Dini baada ya kumalizika kwa hafla ya Ufunguzi wa Masjid Al Noor Unguja Ukuu Kaepwani Wilaya ya Kati Mkoa wa Kusini Unguja leo 26-11-202.na (kushoto kwa Rais) Mbunge wa Jimbo la Tunguu Zanzibar Mhe Khalifa Salum Suleiman.(Picha na Ikulu)


Previous articleSIMBA WATAJA KIINGILIO CHA RED ARROWS
Next articleRAIS MUSEVENI WA UGANDA KUZURU TANZANIA
Hughes Dugilo is a Writer, News Producer, Video-Photographer Journalist, and Video Editor experienced for 20 years now performing in News, Documentary, Advertisements and Television Programs. Aside from all above he own and operate his Blog known as Green Waves Media TZ since 2018.

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here