Home SPORTS KMC, NAMUNGO ZATOSHANA NGUVU

KMC, NAMUNGO ZATOSHANA NGUVU


Na: Mwandishi wetu.

TIMU ya KMC leo imetoka 1-1dhidi ya  Namungo katika mchezo wa ligi kuu Tanzania bara uliochezwa katika dimba la Ilulu mjini Lindi.

Bao la KMC limefungwana  Charles Ilamfya katika dakika ya  dakika 30, kabla ya Shiza Kichuya kuisawazishia Namungo FC dakika ya 43 kwa penalti.

Mchezo mwingine uliopigwa Uwanja wa Nyankumbu, Juma Luizio alianza kuifungia Mbeya City dakika ya 45, kabla ya George Mpole kuwasawazishia wenyeji Geita dakika ya 57.

Namungo inafikisha pointi tano, KMC pointi mbili sawa na Geita Gold na Mbeya City pointi sita baada ya timu zote kucheza mechi nne.

Previous articleSPIKA NDUGAI AZITAKA ASASI ZA KIRAIA KUSHIRIKIANA NA SERIKALI KULETA MAENDELEO, AONYA MIGONGANO
Next articleSPIKA JOB NDUGAI AZITAKA ASASI ZA VIJANA KUSHIRIKIANA NA KAMATI ZA BUNGE.
Hughes Dugilo is a Writer, News Producer, Video-Photographer Journalist, and Video Editor experienced for 20 years now performing in News, Documentary, Advertisements and Television Programs. Aside from all above he own and operate his Blog known as Green Waves Media TZ since 2018.

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here