Home LOCAL PSSSF YAWANOA WASTAAFU WATARAJIWA JUU YA MATUMIZI SAHIHI YA FEDHA.

PSSSF YAWANOA WASTAAFU WATARAJIWA JUU YA MATUMIZI SAHIHI YA FEDHA.


Meneja wa mafao mfuko wa hifadhi ya jamii kwa watumishi wa serikali(PSSSF) Mkehenge Ramadhani akiongea na waandishi wa habari katika semina yao kwa wastaafu watarajiwa mkoani Arusha.

Mkuu wa Wilaya ya Arusha Sophia Mjema akiongea na waandishi wa habari baada ya kufungua semina kwa wastaafu watarajiwa mkoa wa Arusha iliyoandaliwa na PSSSF.    
Meneja mwandamizi wa wa wateja binafsi wa benki ya NMB Ally Ngingite alikieleza jinsi benki hiyo inavyowajali wastaafu.

Lempere Oloije mstaafu mtarajiwa kutoka mamlaka ya hifadhi ya Ngorongoro akielezea umuhimu wa mafunzo hayo

Na: Namnyak Kivuyo, Arusha.

Mfuko wa hifadhi ya jamii kwa watumishi wa umma(PSSSF) imetoa mafunzo kwa watumishi 350 kutoka wilaya zote za mkoa wa Arusha wanatarajiwa kustaafu katika kipindi cha mwaka 2021/2023   ili kuweza kutumia fedha zao vizuri wanapostaafu pamoja kuepuka matapeli.

Akifungua semina hiyo ya siku mbili ya kuwapa elimu ya uwekezaji kwa maisha endelevu baada ya kustaafu mkuu wa wilaya ya Arusha Sophia Mjema alisema kuwa  kumekuwepo na tatizo la wastaafu kutapeliwa fedha zao pindi wanapostaafu huku wengine wakitumia fedha hizo bila mpangilio na mahesabu na kuto kujua kuwa wanavyotumia fedha hizo zinaisha.
 

Mjema aliwataka wastaafu hao kuacha kuangalia familia za watoto wao na kujiendeleza wao binafsi kwani muda wao wakuangalia familia zinazojiendeleza umeisha na uliobaki nikujijali wenyewe  na kuangalia namna watakavyotumia fedha hizo hadi pale ambapo watapoteza maisha.

Aidha aliwataka pindi wanapopata fedha hizo wazitumie kwa ajili ya kujenga maendeleo ya nchi na taifa kwa ujumla huku wakijitahidi kujiendeleza kwa kuwekeza katika kilimo biashara ,ufugaji na mambo mengine mengi  huku akibanisha kuwa fedha wanazopewa sio nyingi maana aziongezeki bali zinapungua kwa iyo ni vyema wakatumia vyema.

Alisema kuwa ana imani semina hii itasaidia kuwaondolea  matatizo  ambayo wastaafu wamekuwa nayo moja wapo ikiwa ni matumizi sahihi ya fedha na kuepuka kutapeliwa na pia  fedha za wastaifu zitatumika vizuri kuongeza pato la wastaafu.

“Naimani mkitoka hapa hakuna atakayedanganyika tena baada ya semina, zingatieni mkitoka hapa mjue mnaenda kufanya nini ili msiende kubabaishwa wala kuyumbishwa,” Alisema.

Kwa upande wake meneja wa  mafao mfuko wa hifadhi ya jamii (PSSSF) Mkehenge Ramadhani alisema kuwa mfuko wao umeanza kutoa mafunzo hayo baada ya kuona matatizo mengi ambayo wastaafu wanakutana nayo hasa ya kutapeliwa nakutumia vibaya fedha zao baada ya kustaafu jambo ambalo linawafanya kuanza kuangaika baada ya muda mfupi wa kustaafu.


Alisema waliona ni vyema wakawapa mafunzo kwaajili ya kuwaandaa kwa maisha  ya baadaye ambapo  zoezi hilo lilifunguliwa rasmi mkoani Dodoma na linatarajiwakufanyika katika mikoa yote hapa nchini na  zaidi ya wastaafu 8000  wanaotarajia  kustaafu  watapatiwa elimu hiyo kwani zoezi hilo ni endelevu.

Naye meneja mwandamizi  wateja binafsi na maalum wakiwemo wastaafu kutoka benki ya NMB ambao ni mmoja kati ya  wathamini wa mafunzo hayo Ally Ngingite alisema kuwa benki yao inawajali sana wastaafu na ndio maana wakaanzisha huduma mbalimbali zinazowahusu ikiwemo kuwapa mikopo wastaafu ,upatikanaji wa fedha kirahisi kwa maana ya mitaji pamoja na kuwapa bima ya afya.

“Katika eneo la uwekezaji kwa wastaafu kuna akaunti maalum ambazo hazina makato na zitawezesha wateja wetu wastaafu  kujiekea amana na  akiba za muda mfupi na mrefu ambazo wataweza kutumia Kama dhamana ya kuchukulia mikopo kwaajili ya mitaji kwahiyo mtaona tumejikita kuhakikisha kwamba wastaafu hawa  wanaenda kufurahiya maisha yao katika kujiongezea kipatoka kwenye kilimo, biashara za ujasiriliamali na nyinginezo kwasababu NMB tunaamini kuwa kustaafu sio mwisho wa maisha,” Alisema.

Mmoja wastaafu watarajiwa  kutoka mamlaka ya hifadhi ya Ngorongoro Lempere Oloije alisema kuwa semina hii itawasaidia  kupata elimu ambayo itawasaidia kuendelea maisha baada ya kustaafu kwani watajua namna ya kutumia fedha za mafao watakapozipata.

Previous articleKITUO CHA KUPOZA UMEME KUJENGWA KONGWA.
Next articleSERIKALI YATOA MAFUNZO YA UKUSANYAJI MAPATO KWA HALMASHAURI NNE JIJINI ARUSHA.

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here