![]() |
Waziri wa Fedha na Mipnago Mhe.Dkt.Mwigulu Nche,ba akiwasilisha bungeni taarifa ya hali ya uchumi na Taifa kwa mwaka 2020 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa wa Mwaka 2021/22. UTANGULIZI.
MWENENDO WA HALI YA UCHUMI KWA MWAKA 2020
Uchumi wa Dunia
Uchumi wa Afrika na Kikanda
Uchumi wa Taifa Pato la Taifa
Mwenendo wa Bei
Utekelezaji wa Sera ya Fedha 2020/21
Ujazi wa Fedha na Karadha
Mwenendo wa Mikopo kwa Sekta Binafsi
Ukuzaji Rasilimali
Sekta ya Nje
Akiba ya Fedha za Kigeni
Mwenendo wa Thamani ya Shilingi
Deni la Serikali
MAFANIKIO YA UTEKELEZAJI WA MPANGO WA MAENDELEO WA TAIFA KWA KIPINDI CHA 2016/17 – 2020/21
Bandari za Maziwa Makuu: Kukamilika kwa ujenzi wa magati ya Nyamirembe, Magarine, Lushamba, Ntama na Mwigobero katika Ziwa Victoria; kukamilika kwa ujenzi wa magati ya Sibwesa na Kabwe pamoja na kuendelea na ujenzi wa Bandari za Karema, Ujiji, Kibirizi na Lagosa katika Ziwa Tanganyika; na kukamilika kwa ujenzi wa sakafu ngumu katika bandari ya Kiwira na Itungi katika Ziwa Nyasa.
Ziwa Victoria na Tanganyika: Kukamilika kwa ukarabati wa meli mbili (2) za New Butiama Hapa Kazi Tu na New Victoria Hapa Kazi Tu; kuendelea na ujenzi wa meli mpya ya MV Mwanza Hapa kazi Tu yenye uwezo wa kubeba abiria 1,200 na tani 400 za mizigo ambao umefikia asilimia 74; na kukamilika kwa ujenzi wa chelezo cha kujengea na kukarabati meli katika Bandari ya Mwanza chenye uwezo wa kubeba meli au chombo chenye uzito kuanzia tani moja (1) hadi tani 4,000. Ziwa Nyasa: Kukamilika kwa ujenzi wa matishari mawili (2) yenye uwezo wa kubeba tani 1,000 kila moja; na kukamilika na kuanza kufanya kazi kwa meli moja mpya ya MV Mbeya II yenye uwezo wa kubeba abiria 200 na tani 200 za mizigo.
Kilimo: Kujengwa na kuboreshwa kwa miundombinu ya umwagiliaji hivyo kuongeza eneo la kilimo cha umwagiliaji kutoka hekta 461,376 mwaka 2015 hadi hekta 694,715 mwaka 2020; kukamilika kwa ujenzi na ukarabati wa skimu 17 za umwagiliaji zenye ukubwa wa hekta 8,536 kupitia ASDP II na skimu tano (5) za Kigugu – Mvomero (hekta 195), Msolwa Ujamaa (hekta 40), Njage – Kilombero (hekta 75), Mvumi – Kilosa (hekta 249) na Kilangali Seed Farm – Kilosa (hekta 400) kupitia mradi wa kuongeza uzalishaji wa mpunga – Expanded Rice Production Project (ERPP); kuongezeka kwa uzalishaji wa mbegu bora kutoka tani 36,614 mwaka 2015 hadi tani 76,726 mwaka 2020; na kukamilika kwa ujenzi wa maabara ya mbegu katika makao makuu ya Wakala wa Mbegu za Kilimo – Morogoro. Mifugo: Kuimarishwa kwa Kituo cha Taifa cha Uhimilishaji kilichopo Usa River Arusha kwa kununua kifaa (Chiller) kwa ajili ya mtambo wa kuzalisha kimiminika cha naitrojeni; kujengwa kwa viwanda vipya vya kimkakati vya nyama vya Tanchoice (Pwani), Elia Food Oversees Limited (Arusha) na Binjiang Company Limited (Shinyanga); kujengwa kwa kiwanda cha maziwa cha Galaxy Food and Beverage Company Limited (Arusha); kujengwa kwa kiwanda cha kuzalisha chanjo cha Hester Bioscience Africa Limited (Pwani) chenye uwezo wa kuzalisha chanjo aina 37; kuendelea kuboresha huduma za malisho ya mifugo na majosho; na kuendelea na ukamilishaji wa ujenzi wa machinjio ya kisasa Vingunguti. Uvuvi: Kuongezeka kwa uvunaji wa samaki katika maji ya asili kutoka tani 362,645 zenye thamani ya shilingi trilioni 1.48 mwaka 2015/16 hadi tani 497,567 za samaki zenye thamani ya shilingi trilioni 2.34 mwaka 2019/20; kuongezeka kwa usindikaji wa minofu ya samaki aina ya Sangara kutoka tani 23,000.6 mwaka 2015/16 hadi tani 27,596.3 mwaka 2019/20; kuongezeka kwa huduma za usafirishaji wa mazao ya uvuvi kwenda masoko ya Ulaya ambapo katika mwaka 2019/20, jumla ya tani 777.8 za mabondo zilisafirishwa; kuongezeka kwa mauzo ya samaki na mazao ya uvuvi nje ya nchi kutoka mauzo yenye thamani ya shilingi bilioni 379.3 mwaka 2015/16 hadi shilingi bilioni 506.2 mwaka 2019/20; na kuendelea na maandalizi ya ujenzi wa Bandari ya Uvuvi (Mbegani) na ununuzi wa meli nne (4) za uvuvi.
MPANGO WA MAENDELEO WA TAIFA WA MWAKA 2021/22 Malengo na Shabaha za Uchumi Jumla kwa Mwaka 2021/22
Miradi ya Kipaumbele kwa Mwaka 2021/22
Uendelezaji wa Miundombinu
Aidha, Serikali itaendelea na ujenzi na ukarabati wa barabara za kupunguza msongamano za Jijini Dar es Salaam (km 138.5) pamoja na barabara za mikoa, kuboresha miundombinu ya mabasi yaendayo haraka kwa awamu zote nne, ujenzi wa barabara za juu (Flyover) Jijini Dar es Salaam, barabara za mzunguko katika Jiji la Dodoma pamoja na barabara za vijijini na mijini kupitia Wakala ya Barabara za Vijijini na Mijini (TARURA). Vilevile, Serikali itaendelea na ujenzi wa madaraja makubwa yakiwemo madaraja ya New Wami (Pwani), Kitengule (Kagera), Kirumi (Mara) na Mkenda (Ruvuma).
Vihatarishi vya Utekelezaji wa Mpango wa Mwaka 2021/22
Mikakati mingine ni pamoja na: Kuhamasisha uwekezaji wa ndani katika kujenga viwanda vya kuzalisha pembejeo za kilimo, ikijumuisha kuimarisha kilimo kinachohimili mabadiliko ya tabianchi – Climate Smart Agriculture; kuongeza ubora wa bidhaa zinazozalishwa ndani ili kuongeza ushindani katika masoko ya nje; kuimarisha mifumo ya utatuzi wa migogoro kwa njia ya majadiliano ili kuzuia matukio yanayoweza kuhatarisha amani nchini; na kuendelea kuimarisha ushirikiano wa kibiashara na maendeleo ya kiuchumi ya kikanda na kimataifa. Ugharamiaji wa Mpango 2021/22
Ufuatiliaji, Tathmini na Utoaji wa Taarifa za Utekelezaji
MAJUMUISHO
HITIMISHO
|
WAZIRI DKT. NCHEMBA AWASILISHA BUNGENI TAARIFA ZA HALI YA UCHUMI NA MPANGO WA MAENDELEO
Thank you for reading this post, don't forget to subscribe!