Home LOCAL DKT.NDUGULILE AIPONGEZA TCRA KWA UBUNIFU WA MIFUMO WEZESHI YA HUDUMA ZA MAWASILIANO.

DKT.NDUGULILE AIPONGEZA TCRA KWA UBUNIFU WA MIFUMO WEZESHI YA HUDUMA ZA MAWASILIANO.

Waziri wa Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Mhe. Dkt. Faustine Ndugulile (mbele, kulia) akiwahimiza Wataalamu kutoka TCRA kuhusu uboreshaji wa Mifumo ya Huduma za Mawasiliano Nchini.

Waziri wa Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Mhe. Dkt. Faustine Ndugulile akipokelewa na Mkurugenzi Mkuu Dkt. Jabiri Bakari, pamoja na Wakuu wa Idara na vitengo vya Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania TCRA alipotembelea Makao Makuu ya Taasisi hiyo, Tarehe 04/06/2021.

Waziri wa Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Mhe. Dkt. Faustine Ndugulie (Kushoto) akizungumza na Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) Dkt. Jabiri Bakari (Kulia) mara baada ya kuwasili Makao Makuu ya TCRA.
Waziri wa Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Mhe. Dkt. Faustine Ndugulile (Kushoto) akisikiliza wasilisho kuhusu Kituo cha kuratibu Majanga ya kimtandao (TZ CERT) lililotolewa na Mkuu wa Kitengo hicho Mhandisi. Darius Luhaga (Kulia).

Na: Mwandishi Wetu.

SERIKALI imehimiza uboreshaji wa Mifumo mbalimbali ya usimamizi wa huduma za Mawasiliano ili kuhakikisha kunakuwa na Usalama na Ubora wa Huduma Nchini.   

Akizungumza katika ziara ya kutembelea mifumo hiyo kwenye Taasisi ya Udhibiti, Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), jijini Dar Es salaam, , Waziri wa Mawasiliano na Teknolojia ya Habari Mhe. Dkt. Faustine E. Ndugulile (Mb) amesema Wananchi wanatarajia kupata huduma bora zenye usalama.

“Upatikanaji wa huduma Bora, za Uhakika na Salama nijambo la msingi sana kwa ajili ya maendeleo ya Wananchi na Taifa” amesema Mhe. Ndugulile.

Katika ziara hiyo Mhe. Ndugulile alipokelewa na Mkurugenzi Mkuu wa TCRA Dkt. Jabiri K. Bakari na Menejimenti alipotembelea mifumo ya udhibiti wa Mawasiliano.

Dkt. Ndugulile aliipongeza TCRA kwa ubunifu wa kujenga Mifumo  Wezeshi kwa huduma mbalimbali za Mawasiliano Nchini, ambapo alisema uboreshaji wake nimuhimu sana.

Baadhi ya mifumo aliyotembelea Mhe. Waziri ni Mfumo wa Usimalizi na Udhibiti wa Masafa ya Redio na Televisheni na Kituo cha Kuratibu Majanga ya Kimtandao (TZ-CERT).  TZ-CERT pia itatoa ushuri wa kitaalam namna bora wa kudhibiti na kupambana ya majanga mbalimbali ya Kimtandao kwa Taasisi na makampuni mbalimbali hapa Nchini.

Mhe. Waziri pia alitembelea    Kituo cha Huduma kwa Wateja ambapo alihimiza TCRA kuendelea kushirikiana na Taasisi zingine zikiwemo za Kiudhibiti kama Bank Kuu ya Tanzania (BOT).

Previous articleNAIBU WAZIRI AIPONGEZA TANROADS KUWATUMIA WAKANDARASI WAZAWA
Next articleKUTOKA MEZA YA MAGAZETI ASUBUHI YA LEO J.TATU JUNI 7-2021

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here