Home BUSINESS TANZANIA KUIMARISHA USHIRIKIANO NA JAPAN, IFAD

TANZANIA KUIMARISHA USHIRIKIANO NA JAPAN, IFAD

           Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (Mb) (kulia), akiagana na Balozi wa Japan nchini Tanzania, Mhe. Yoichi Mikami, aliyefika kwa ajili ya kujitambulisha na kujadili masuala mbalimbali ya ushirikiano wa kiuchumi na maendeleo kati ya Tanzania na Japan, katika Ofisi ya Waziri wa Fedha, Treasury Square, jijini Dodoma.

Thank you for reading this post, don't forget to subscribe!


Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (Mb), akizungumza jambo wakati wa kikao chake na Balozi wa Japan nchini Tanzania, Mhe. Yoichi Mikami (hayupo pichani), aliyefika kwa ajili ya kujitambulisha na kujadili masuala mbalimbali ya ushirikiano wa kiuchumi na maendeleo kati ya Tanzania na Japan, katika Ofisi ya Waziri wa Fedha, Treasury Square, jijini Dodoma.


Balozi wa Japan nchini Tanzania, Mhe. Yoichi Mikami, akizungumza jambo wakati wa kikao chake na Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (Mb) (hayupo pichani), alipofika kwa ajili ya kujitambulisha na kujadili masuala mbalimbali ya ushirikiano wa kiuchumi na maendeleo kati ya Tanzania na Japan, katika Ofisi ya Waziri wa Fedha, Treasury Square, jijini Dodoma.


Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (Mb) (Katikati), Balozi wa Japan nchini Tanzania, Mhe. Yoichi Mikami (wa tatu kushoto), Naibu Waziri wa Fedha, Mhe. Mhandisi Mshamu Ali Munde (Mb)(wa tatu kulia), Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Fedha, Bi. Amina Khamis Shaaban (wa pili kulia), Kaimu Kamishna wa Idara ya Uchambuzi wa Sera, Wizara ya Fedha, Dkt. Remidius Ruhinduka (wa pili kushoto), Afisa wa Siasa, Utamaduni na Uhusiano wa Umma, ubalozi wa Japan nchini, Bi. Yoshino Shibata (kushoto) na Afisa kutoka Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Bw. Frank Mhina (kulia), wakiwa katika picha ya pamoja, baada ya kikao cha Mhe. Balozi Omar na Mhe. Mikami, kilichofanyika katika ofisi za Wizara ya Fedha, Treasury Square jijini Dodoma


Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (Mb) (kulia), akiagana na Mkurugenzi Mkazi wa Mfuko wa Kimataifa wa Maendeleo ya Kilimo (IFAD), Bw. Sakphouseth Meng, baada ya kukutana na kufanya mazungumzo katika ofisi za Wizara ya Fedha, Treasury Square jijini Dodoma, ambapo pamoja na mambo mengine Mhe. Balozi Omar, aliishukuru IFAD kwa mchango wake katika maendeleo ya kilimo nchini.


Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (Mb), akizungumza jambo wakati wa kikao chake na Mkurugenzi Mkazi wa Mfuko wa Kimataifa wa Maendeleo ya Kilimo (IFAD), Bw. Sakphouseth Meng (hayupo pichani), katika ofisi za Wizara ya Fedha, Treasury Square jijini Dodoma, ambapo wawili hao walijadiliana masuala mbalimbali ya ushirikiano katika kukuza maendeleo ya Sekta ya kilimo na miundombinu ya nishati.


Mkurugenzi Mkazi wa Mfuko wa Kimataifa wa Maendeleo ya Kilimo (IFAD), Bw. Sakphouseth Meng, akizungumza jambo wakati wa kikao chake na Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (Mb), (hayupo pichani), katika ofisi za Wizara ya Fedha, Treasury Square jijini Dodoma, ambapo wawili hao walijadiliana masuala mbalimbali ya ushirikiano katika kukuza maendeleo ya Sekta ya kilimo na kuongeza tija katika sekta hiyo.


Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (Mb) (katikati), akizungumza jambo wakati wa kikao chake na Mkurugenzi Mkazi wa Mfuko wa Kimataifa wa Maendeleo ya Kilimo (IFAD), Bw. Sakphouseth Meng (hayupo pichani), katika ofisi za Wizara ya Fedha, Treasury Square jijini Dodoma, ambacho kilijadili masuala mbalimbali ya ushirikiano katika kukuza maendeleo ya Sekta ya kilimo kwa ujumla wake na kwa upande wa kuongeza uzalishaji na tija katika uzalishaji. Wengine katika picha ni Naibu Waziri wa Fedha, Mhe. Mhandisi Mshamu Ali Munde (Mb)(Kushoto) na Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Fedha, Bi. Amina Khamis Shaaban (Kulia).


Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (Mb) (Kulia), akiteta jambo na Mkurugenzi Mkazi wa Mfuko wa Kimataifa wa Maendeleo ya Kilimo (IFAD), Bw. Sakphouseth Meng, wakati wakibadilishana kadi kwa ajili ya mawasiliano baada ya kikao chao kilichofanyika katika ofisi za Wizara ya Fedha, Treasury Square jijini Dodoma, ambacho kilijadili masuala mbalimbali ya ushirikiano katika kukuza maendeleo ya Sekta ya kilimo kwa ujumla wake na kwa upande wa kuongeza uzalishaji na tija katika kilimo.


Naibu Waziri wa Fedha, Mhe. Mhandisi Mshamu Ali Munde (Mb)(Kulia) akiteta jambo na Mkurugenzi Mkazi wa Mfuko wa Kimataifa wa Maendeleo ya Kilimo (IFAD), Bw. Sakphouseth Meng, baada ya kikao cha Mkurugenzi huyo na Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (Mb) (hayupo pichani), kilichofanyika katika ofisi za Wizara ya Fedha, Treasury Square jijini Dodoma.  


Waziri wa Fedha, Mhe. Balozi Khamis Mussa Omar (Mb) (Katikati), Mkurugenzi Mkazi wa Mfuko wa Kimataifa wa Maendeleo ya Kilimo (IFAD), Bw. Sakphouseth Meng, wakiwa katika picha ya pamoja baada ya kikao chao kilichofanyika katika Ofisi za Wizara ya Fedha, Treasury Square jijini Dodoma. Wengine katika picha ni Naibu Waziri wa Fedha, Mhe. Mhandisi Mshamu Ali Munde (wa nne kulia), Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Fedha, Bi. Amina Khamis Shaaban (wa tatu kushoto), Kamishna Msaidizi wa Idara ya Usimamizi wa Madeni, Wizara ya Fedha, Bw. Omary Khama (wa pili kulia), Mkurugenzi Msaidizi Idara ya Sheria, Wizara ya Fedha, Bi. Zawadi Maginga (kulia), Mratibu Mkazi wa IFAD, Bi. Jacqueline Machangu-Motcho (wa tatu kulia), Wachumi kutoka Idara ya Fedha za Nje Wizara ya Fedha, Bw. John Kuchaka (wa pili kushoto) na Bi. Zahra Michuzi (kushoto).

(Picha na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini, WF, Dodoma)