Home LOCAL UJUMBE WA MADAKTARI WA KICHINA WALIOMALIZA MUDA WA KAZI HAPA NCHINI

UJUMBE WA MADAKTARI WA KICHINA WALIOMALIZA MUDA WA KAZI HAPA NCHINI

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Hussein Ali Mwinyi (kulia) alipokuwa akimkabidhi zawadi  Kiongozi wa Ujumbe wa Madaktari wa Kichina Dr.Zhao Xiaojun   wakati wa kuagana na  Ujumbe wa Madaktari hao wa  Kichina  32 waliomaliza muda   wao wakutoa huduma  mbali mbali  katika Hospitali za Mnazi Mmoja na Abdalla Mzee Pemba,hafla ya kuagana ilifanyika leo  ukumbi wa  Ikulu Jijini Zanzibar. [Picha na Ikulu] 11Sept 2023.
Baadhi ya Madaktari wa kichina na Mkalimani wakifuatilia kwa makini sherehe ya Kuagwa kwao waliofika Ikulu Jijini Zanzibar leo Kuagana na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Hussein Ali Mwinyi (hayupo pichani).[Picha na Ikulu] 11Sept 2023.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Hussein Ali Mwinyi (katikati) akimsikiliza Kiongozi wa  Madaktari wa Kichina Dr.Zhao Xiaojun (kulia aliyesimama) wakati akitoa shukurani zake leo kwa Ushirikiano walioupata katika  huduma walizozitoa katika Hospitali za Zanzibar,wakati hafla ya kuagana wa lipofika Ikulu Jijini Zanzibar . [Picha na Ikulu] 11Sept 2023.
Viongozi wa Ujumbe wa Madaktari wa Kichina wamsikiliza  Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Hussein Ali Mwinyi (hayupo pichani) alipokuwa akitoa hutuba yake wakati walipofika kumuaga Rais leo Ikulu Jijini Zanzibar. [Picha na Ikulu] 11Sept 2023.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Hussein Ali Mwinyi (kulia) alipokuwa akitoa hutuba yake wakati wa kuagana na  Ujumbe wa Madaktari wa Kichina 32 waliuomaliza muda ambao wakitoa huduma katika Hospitali za Mnazi Mmoja na Abdalla Mzee Pemba,mazungumzo yalifanyika leo walipofika  Ikulu Jijini Zanzibar. [Picha na Ikulu] 11Sept 2023.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Hussein Ali Mwinyi   alipokuwa akitoa hutuba yake wakati wa kuagana na  Ujumbe wa Madaktari wa Kichina (hawapo pichani) 32 waliomaliza muda ambao wakitoa huduma katika Hospitali za Mnazi Mmoja na Abdalla Mzee Pemba,mazungumzo yalifanyika leo walipofika  Ikulu Jijini Zanzibar. [Picha na Ikulu] 11Sept 2023.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Hussein Ali Mwinyi (kulia) alipokuwa akimkabidhi zawadi  Kiongozi wa Ujumbe wa Madaktari wa Kichina Dr.Zhao Xiaojun   wakati wa kuagana na  Ujumbe wa Madaktari hao wa  Kichina  32 waliomaliza muda   wao wakutoa huduma  mbali mbali  katika Hospitali za Mnazi Mmoja na Abdalla Mzee Pemba,hafla ya kuagana ilifanyika leo  ukumbi wa  Ikulu Jijini Zanzibar. [Picha na Ikulu] 11Sept 2023.
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Hussein Ali Mwinyi (kulia) alipokuwa akipokea  zawadi  kutoka kwa Kiongozi wa Ujumbe wa Madaktari wa Kichina Dr.Zhao Xiaojun   wakati wa kuagana na  Ujumbe hguo wa Madaktari 32 waliomaliza muda  wa kutoa  huduma  mbali mbali  katika Hospitali za Mnazi Mmoja na Abdalla Mzee Pemba,katika hafla  iliyofanyika leo  ukumbi wa  Ikulu Jijini Zanzibar. [Picha na Ikulu] 11Sept 2023.
Zanzibar, 11 Septemba, 2023

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Hussein Ali Mwinyi ameishukuru Serikali ya China kwa ushirikiano wanaoendelea kuutoa kwa Tanzania ikiwemo Zanzibar kwenye masuala mbalimbali ya maendeleo.

Dk. Mwinyi ametoa shukurani hizo Ikulu, Zanzibar alipowakabidhi vyeti na medali timu ya madaktari 32 kutoka China waliohudumu kwenye hospitali za Zanzibar kwa kipindi cha mwaka mmoja na kuwaaga baada ya kumaliza muda wao nchini.

Rais Dk. Mwinyi amesema, Zanzibar imenufaika na fursa nyingi kutoka China kupitia sekta mbalimbali za maendeleo ikiwemo Afya hususan kupokea timu za madaktari bingwa wanaofika nchini kubadilishana uzoefu na wazawa hali aliyoieleza imeimarisha uhusiano mwema uliopo baina yao pamoja na kujifunza uzoefu wa masuala mbalimbali ya afya.

Dk. Mwinyi alieleza Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar imeendeleza maeneo mengi ya afya kwa kujenga hospitali zenye vifaa tiba vya kisasa, kuboresha miundombinu na kuongeza hospitali za wilaya na mikoa pamoja na kuifanyia matenegezo makubwa hospitali ya Mnazi Mmoja.

Aidha, Rais Dk. Mwinyi ameshukuru kazi kubwa iliyofanywa na timu hiyo ya madaktari 32 kipindi chote walichohudumu Zanzibar na kusema Serikali ilnajivunia kuwepo kwao.

Akizungumza kwenye hafla hiyo Waziri wa Afya Zanzibar Nassor Ahmed Mazrui ametoa Shukraani zake kwa timu ya madaktari hao nakueleza ushirikiano uliopo baina ya China na Zanzibar umedumu kwa miaka 60 sasa.

Naye, Kaimu Katibu Mkuu Wizara ya Afya Dk. Amour Suleiman Mohammed alisema timu hiyo ya madaktari bingwa kutoka China iliwasili nchini Septemba 26 mwaka 2022 na Septemba 26 mwaka huu inatarajiwa kurejea kwao.

Alisema timu hiyo ilitoa msaada wa kitabibu kwa wananchi wa Unguja na Pemba kwa magonjwa ya macho, meno, mkojo, figo, huduma za X- ray, pia ilifanya upasuaji kwa wagonjwa zaidi ya 50 kwa maradhi tofauti.

Kiongozi mkuu wa timu ya madaktari hao 32 , Dk. Zhao Xiaojun alishukuru Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kwa ushirikiano ilioutoa kipindi chote na kueleza Zanzibar ni visiwa vyenye upendo, amani na mshikamano kwa wenyeji na wageni.

“Kamwe hatutasahau uzuri na haiba ya mandhari ya visiwa vya Zanzibar vilivyopambwa kwa maumbile ya anga la buluu, fukwe nyeupe, uzuri wa mwanga wajua linapochomoza, kijani cha minazi na ukarimu wa watu wake, yote haya tutayakosa baada ya kuondoka Zanzibar” kwa hisia alisema.

Hata hivyo, timu ya madaktari hao ilimuahidi Dk. Mwinyi kuendeleza ushirikiano uliopo baina yao.

Previous articleKAMATI YA BUNGE YARIDHISHWA NA UTENDAJI WA TMDA
Next articleNIC YAFANYA MAGEUZI MAKUBWA KATIKA KIPINDI CHA MIAKA MITATU
Hughes Dugilo is a Writer, News Producer, Video-Photographer Journalist, and Video Editor experienced for 20 years now performing in News, Documentary, Advertisements and Television Programs. Aside from all above he own and operate his Blog known as Green Waves Media TZ since 2018.

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here