Home LOCAL WATU 206 WATHIBITIKA KUWA NA VIRUSI VYA CORONA NDANI YA WIKI MOJA

WATU 206 WATHIBITIKA KUWA NA VIRUSI VYA CORONA NDANI YA WIKI MOJA

Na.WAF,Mara

Waziri wa Afya Mhe. Ummy Mwalimu amesema hali ya UViKO-19 nchini katika kipindi cha tarehe 29 Januari hadi 4 Februari, 2022, jumla ya 6,938 walipimwa na watu 206 walithibitika kuwa na Virusi vya Corona ndani ya wiki moja.

Waziri Ummy ameyasema hayo leo wakati ya ziara ya Rais Samia Suluhu Hassan kwenye hospitali ya Rufaa ya Kumbukumbu ya Mwl.J.K Nyerere Mkoani Mara.

Amesema wagonjwa wapya 71 walilazwa, kati ya hao asilimia 97% walikuwa hawajachanjwa.Na kwa siku ya tarehe 4 Februari, wagonjwa mahututi 11 waliripotiwa na wote sawa na 100% hawakuwa wamepata chanjo dhidi ya UVIKO-19. 

Aidha, amesema wagonjwa watatu (3) wameripotiwa kuwa mahututi na wote (100%) hawajachanjwa. 

Kwa upande wa vifo Waziri Ummy amesema kwa tarehe 29 Januari hadi 4 Februari,2022, Jumla ya vifo vitatu (3) vimeripotiwa  kutoka mikoa ya Dodoma (1), Morogoro (1) na Manyara (1), vifo vyote (100%) vilivyoripotiwa vilikuwa vya wagonjwa ambao hawakuchanjwa.

Previous articleCHAMA AAMSHA SHANGWE ZA MASHABIKI WA SIMBA KWA MKAPA
Next articleSENEGAL YANYAKUA UBINGWA WA AFCON 2022, YAICHAPA MISRI KWA PENALT 4-2
Hughes Dugilo is a Writer, News Producer, Video-Photographer Journalist, and Video Editor experienced for 20 years now performing in News, Documentary, Advertisements and Television Programs. Aside from all above he own and operate his Blog known as Green Waves Media TZ since 2018.

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here