Home Uncategorized MATUKIO KATIKA PICHA CHONGOLO ZIARANI MKINGA TANGA

MATUKIO KATIKA PICHA CHONGOLO ZIARANI MKINGA TANGA


Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi Ndugu Daniel Chongolo akihutubia wakazi wa shina namba 3 tawi la Mapambano Kijiji cha Magani wilaya ya Mkinga mkoani Tanga.

Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi Ndugu Daniel Chongolo akiteta jambo na Mwenyekiti wa shina namba 3 tawi la Mapambano Ndugu Mnyatani Msema (kulia) mara baada ya kutembelea na kuzungumza na wakazi wa shina hilo lililopo Kijiji cha Magani wilaya ya Mkinga mkoani Tanga.

Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi Ndugu Daniel Chongolo akimsikiliza Mkuu wa Wilaya ya Mkinga Kanali Maulid Hassan Surumbu mara baada ya kuwasili wilayani hapo akitokea wilaya ya Pangani, katikati ni Mkuu wa Wilaya ya Pangani Ndugu Ghalibu Ringo.

Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi Ndugu Daniel Chongolo akipata maelezo ya maendeleo ya mradi wa ujenzi wa Chuo Cha Veta Mkinga kutoka kwa Mkuu wa Chuo cha Veta Tanga Ndugu Gideon Ole Laiombe (kulia), kushoto ni Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Mkinga Ndugu Ismail Kasomo.

Previous articleRC SHIGELLA AZIONYA CBWSO’s KUZINGATIA BEI ELEKEZI YA MAJI.
Next articleUMATI MKUBWA WAJITOKEZA ZIARA YA RAIS SAMIA NJOMBE, IRINGA

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here