Home BUSINESS BRELA YATOA HUDUMA YA USAJILI WA BIASHARA KWENYE KONGAMANO LA VIJANA NA...

BRELA YATOA HUDUMA YA USAJILI WA BIASHARA KWENYE KONGAMANO LA VIJANA NA MAENDELEO BENKI DAR.

Afisa wa Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA), Methusela Mahona  akimkabidhi cheti cha usajili wa jina la biashara   Jacqueline Said Sevury, baada ya kusajili  kwa njia ya mtandao  katika   banda la BRELA, wakati wa kongamano la Vijana lililoandaliwa na Benki ya Maendeleo, kongamano hili lillilohusu Ujasiriamali, Uwekezaji na Maendeleo ya Kiuchumi, lilifanyika tarehe 12 Juni, 2021 katika Kanisa la KKKT  Usharika wa Kitunda Relini Jijini Dar es Salaam.

Maafisa wa Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA), Sweetness Madata(kushoto) na Joram Manyika(kulia) wakitoa huduma ya usajili kwa njia ya mtandao  kwa vijana walioshiriki Kongamano  la Vijana na Maendeleo Benki, lililohusu Ujasiriamali, Uwekezaji na Maendeleo ya Kiuchumi. Kongamano hilo lilifanyika katika Kanisa la Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Dayosisi ya Mashariki na Pwani (DMP), Usharika wa Kitunda Relini tarehe 12 Juni, 2021.



Previous articleMEYA JIJI LA DAR ES SALAAM AFUNGUA SEMA PAMOJA NA MAONESHO YA BIDHAA ZA WAJASIRIAMALI.
Next articleTHBUB YATOA TAMKO MAALUM WAKATI WA MAADHIMISHO YA ALBINO

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here