Home LOCAL MAJALIWA ATAKA HATUA ZAIDI ZICHUKULIWE KWA WANAOHUSIKA NA MFUMO WA LUKU.

MAJALIWA ATAKA HATUA ZAIDI ZICHUKULIWE KWA WANAOHUSIKA NA MFUMO WA LUKU.

 

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, amemuagiza Waziri wa Nishati Dkt. Medard Kalemani asiishie kuwasimamisha kwa siku kumi tu meneja wa TEHAMA na wasaidizi wake, bali wakae pembeni hadi hapo uchunguzi zaidi utakapokamilika.
 
Ametoa agizo hilo leo Mei 20, 2021 alipozungumza na Menejementi na Bodi ya Wakurugenzi ya Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) kwenye makao makuu ya zamani Shirika hilo jijini Dar es Salaam.
 
“lazima tufundishane kuwa makini, kila siku lazima tukague vifaa vyetu ili huduma ipatikane muda wote. Hakuna kuwasimamisha kwa siku 10, wakae pembeni hadi timu inayochunguza itakapotoa matokeo.  Inawezekana sio wao tu, Waziri endelea na uchunguzi”
 
Aidha, Waziri Mkuu ameliagiza shirika hilo kuhakikisha wanakuwa na mfumo wa dharura ‘backup’ utakaotumika pindi kunapotokea changamoto za kimfumo
 
“Mmetengeneza usumbufu mkubwa sana, mlijua lazima kuwe na backup lakini hakuna, toka pale tulipoanza kutoa huduma mpaka leo kwanini hakuna backup, hilo ni jukumu lenu”
 
Previous articleKARIBU USOME HABARI MAGAZETI YA LEO ALHAMISI MEI 20-2021
Next articleHOSPITALI ZIMETAKIWA KUWAHUDUMIA WAZEE IPASAVYO.

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here