Home LOCAL MSAMA: WATU WAHESHIMU MAMLAKA TULIYOPEWA NA MUNGU

MSAMA: WATU WAHESHIMU MAMLAKA TULIYOPEWA NA MUNGU

Thank you for reading this post, don't forget to subscribe!

DAR ES SALAAM 

Mkurugenzi wa Kampuni ya Msama Promotion  Alex Msama amesema  wote wanaomsema vibaya Rais wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan kwani kwa kufanya hivyo wanamsema Mwenyezi Mungu ambaye ndiye aliyempa Mamlaka aliyonayo.

Msama ametumia vifungu vya Bibilia kutoka katika Kitabu cha Warumi 13:3 -1 akinukuu, “Kila mtu atii Mamlaka Kuu, Kwa maana hakuna Mamlaka isiyotoka kwa Mungu” hivyo kuwasihi Wananchi wote kuheshimu Mamlaka ambazo zinawaongoza.

Ameyasema hayo Leo Juni, 8, 2025  Jijini Dar-es-Salaam, wakati Akizungumza na waandishiwa habari, na akifafanua kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, ameteuliwa na Mungu kwaajili ya kuwatumikia Watanzania.

Aliongeza kuwa, kwa sasa Rais Samia anakaribia kumaliza kipindi chake, akitarajia kuingia kwenye awamu ya pili. hivto ni muhimu kwa wananchi, hususani wale wanaojihusisha na dini, kumheshimu Rais na mamlaka zake.

“Baadhi ya watu wamekuwa wakiandika jumbe za matusi na kudharau mamlaka, jambo ambalo linapaswa kuacha mara moja. Siasa hazipaswi kuchanganyikana na mambo ya ibada,” alisema Msama. Alionya kwamba miongoni mwa watumishi wa dini, kuna wale wanaojaribu kupeleka siasa ndani ya nyumba za ibada, hali inayohatarisha umoja na amani.
“Siasa si sehemu ya ibada; nyumba za ibada ni mahali pa kumuabudu Mungu, iwe ni kanisani au msikitini. Ikiwa unataka kuzungumzia siasa, basi acha mambo ya dini na uelekee kwenye siasa. Ni muhimu kwa watumishi wa Mungu kuelewa majukumu yao na kujitenga na mambo yasiyofaa,” alisisitiza.
Kwa mujibu wa Msama, ni jukumu la kila mmoja wetu kuheshimu mamlaka na kuzingatia maadili ya kitaifa ili kuhakikisha nchi yetu inakuwa na amani na maendeleo wakati huu wa kuelekea uchaguzi.